Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

Dawa ya gono kwa mwanaume

Dawa ya gono kwa mwanaume

Ugonjwa wa gonorrhea maarufu kama GONO au Kisonono ni ugonjwa wa zinaa ambao husababishwa na Bacteria ambaye kwa kitaalam hujulikana kama Neisseria gonorrhoeae na kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana.

DALILI ZA UGONJWA WA GONO(KISONONO) NI PAMOJA NA;

Kumbuka; Ugonjwa huu wa kisonono kwa asilimia kubwa ni vigumu mwanamke kuonyesha dalili za moja kwa moja hata kama ameambukizwa. Lakini kama akionyesha dalili basi baadhi ya dalili kama hizi hapa chini huweza kutokea.

MIONGONI MWA DALILI AMBAZO HUWEZA KUJIONYESHA KWA MWANAMKE NI PAMOJA NA;

  1. Mwanamke kupatwa na tatizo la maumivu makali wakati wa kufanya mapenzi
  2. Mwanamke kutokwa na maji maji ukeni ambayo yana harufu sana
  3.  Mwanamke kutokwa na ute ute ambayo umechanganyika na usaha ukeni
  4. Kutokwa na damu baada ya kufanya tendo la ndoa
  5. Kupatwa na shida ya blid mara mbili ndani ya mwezi mmoja
  6. Kupatwa na maumivu makali ya tumbo
  7. Joto la mwili kupanda au kuwa na homa
  8. Kuvimba kwenye eneo la mashavu ya uke

DALILI ZA UGONJWA WA KISONONO KWA MWANAUME NI PAMOJA NA;

– Kutokwa na usaha sehemu za Siri

– Kuwashwa kwenye kitundu ambacho mkojo hupita

– Kupatwa na hali ya kuchomwa wakati wa kukojoa ambayo tunasema kwa kitaalam burning sensation

– Mwanaume kupatwa na tatizo la kushindwa kukojoa kabsa au mkojo kugoma kutoka, kitu ambacho huweza kumsababishia maumivu makali pamoja na mahangaiko

– Kukojoa mkojo ambao umechanganyika na Damu

– Joto la mwili kupanda au kuwa na homa

MATIBABU YA UGONJWA WA KISONONO

Ni vizuri kwenda hospital kufanyiwa vipimo kwanza kabla ya dawa, Na baada ya hapo kama utagundulika una tatizo hili basi utapata matibabu sahihi kulingana na ugonjwa wako pamoja na hatua ulipofikia.

TIBA YA KISONONO(Ugonjwa wa zinaa)

Kwa asilimia kubwa Mgonjwa wa kisonono hupewa Dawa ya Cefriaxone 500mg Single dose ambapo ni sindano anachomwa matakoni au sehemu yoyote yenye msuli Kwa kitaalam tunaita Intramuscular Injection(IM).

Epuka matumizi ya dawa hovio pasipo maelekezo na vipimo kutoka kwa wataalam wa afya. Kwani ni hatari kwa afya yako,badala ya kukutibu inaweza kuwa sumu ya kukuua.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.