Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Hadi kufikia sasa miili iliyopatikana ni 87 na yote imeshatambuliwa na Ndugu zao

Serikali ya Tanzania jana Jumapili December 10, 2023, imetoa taarifa kuhusu maendeleo ya hali baada ya maafa ya maporomoko ya tope, mawe, magogo na maji kutoka Mlima Hanang Wilayani Hanang Mkoani Manyara ambapo imesema hadi kufikia sasa miili iliyopatikana ni 87 na yote imeshatambuliwa na Ndugu zao na kuchukuliwa kwa mazishi.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dodoma, Mobhare Matinyi, amesema kwa maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali inagharamia mazishi yote na kutoa mkono wa pole wa Tsh. milioni moja kwa kila mwili ambapo kama Familia imepoteza Watu watano inapewa Tsh. milioni tano.

“Hadi sasa jumla ya majeruhi na Wagonjwa waliopokelewa tangu maafa yatokee ni 139 lakini waliopo Hospitalini hadi leo ni 30, Wagonjwa wengine wote isipokuwa wawili waliofariki wamesharuhusiwa kurejea nyumbani”

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.