Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

BREAKING: Ugonjwa wa ‘Red Eyes’ wahamia Kenya

BREAKING: Ugonjwa wa ‘Red Eyes’ waripotiwa na Kenya

Wataalam wa afya nchini Kenya wanachunguza mlipuko wa maambukizo ya ugonjwa wa macho mekundu “Red eyes”, unaowasumabua wakaazi wa jiji la Mombasa na Kilifi pwani ya nchi hiyo.

Wakazi wameshauriwa kuzingatia kanuni za usafi kama vile kunawa mikono, kuepuka kushiriki vitu vya kibinafsi na kuacha kugusa macho yao.

Wiki iliyopita, mamlaka za afya nchini Tanzania zilitoa tahadhari baada ya kurekodi visa 869 vya ugonjwa huo katika mwezi mmoja, wengi wao wakiwa katika jiji la kibiashara la Dar es Salaam.

Conjunctivitis, pia inajulikana kama ugonjwa mwekundu wa jicho ambapo pia unaifanya sehemu inayolinda macho kuvimba .

Ugonjwa husababishwa na mzio au maambukizi na dalili zake ni kama vile macho kuwa mekundu, uvimbe, machozi au kuwasha.

Wagonjwa wengine wanaweza pia kutoa uchafu kutoka kwa jicho kwa mujibu wa maofisa wa afya.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.