Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Namna ya kuandaa maji salama kwa kutumia kidonge cha Klorini

Weka maji yako kwenye chombo kisafi chenye mfuniko.

Zingatia:maji yakiwa ya tope yachujwe kwanza na kitambaa kisafi kisha yawekwe kwenye chombo chenye mfuniko.

✅Weka kidonge kimoja cha Klorini katika ujazo wa lita 10 za maji au vidonge viwili kwenye ujazo wa lita 20 za maji na kisha funika na tikisa ili ichanganye vizuri.

✅Subiri kwa muda wa dakika 30 na baada ya muda huo unaruhusiwa kunywa maji hayo.

✅Maji yako ya kunywa sasa ni salama .

TAHADHARI:
✅Usimeze kidonge cha Klorini.

✅Vidonge vya Klorini viwekwe mbali na watoto pamoja na mwanga wa jua.

✅Maji ya kunywa yahifadhiwe vizuri na epuka kuchota kwa kutumbukiza kikombe au kata kwa usalama zaidi chombo kitakachotumika kuhifadhia kiwe na koki kuwezesha uchotaji wa maji hayo kwa urahisi.

Forum Manager

Content creator&editor (Ms.Asifiwe)Jukumu langu kwako ni kuhakikisha unapata elimu ya kutosha pamoja na Updates mbali mbali ndani ya http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.