Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
afyatips

Faida za karafuu,Soma hapa kufahamu

Faida za karafuu,Soma hapa kufahamu

Katika Makala hii tumekuandalia faida za karafuu ambazo pengine ulikuwa huzijui kabsa, Kwa kweli, utafiti unaonyesha kwamba karafuu inaweza kuwa na manufaa kadhaa ya afya, ikiwa ni pamoja na kusaidia afya ya ini na kusaidia kuweka Sawa Kiwango cha sukari kwenye damu.

Hapa tumekuchambulia Faida Kadhaa za Karafu ambazo pengine ulikuwa huzifahamu kabsa;

1. Karafuu ina virutubisho muhimu sana mwilini ikiwemo;

  • nyuzi nyuzi(fiber),
  • Vitamins,
  • Pamoja na Madini

Tafiti zinaonyesha kijiko kimoja cha Karafuu huweza kutoa;

Calories: 6
Carbs: 1 g
Fiber: 1 g
Manganese: 55% of the Daily Value (DV)
Vitamin K: 2% of the DV

Madini ya Manganese ni muhimu sana kwenye kusaidia afya ya na utendaji kazi wa Ubongo pamoja na kujenga Mifupa Imara.

2. Karafuu ina kiwango kikubwa cha antioxidants;

Mbali na kusheheni Vitamins na madini,Pia Karafuu ina antioxidants za kutosha,

Antioxidants hizi husaidia kupunguza uwezekano wa mtu kupata magonjwa ya Muda mrefu yaani chronic disease.

Mfano wa antioxidants muhimu sana ndani ya Karafuu ni hii inaitwa eugenol,

Hivo hii husaidia kuboresha afya ya Mwili kwa Ujumla.

3. Karafuu huweza kusaidia kuboresha afya ya Ini

Antioxidants kama vile eugenol husaidia kuzuia uharibifu wa Ini dhidi ya viambato vya Sumu kama vile thioacetamide.

Ingawa pia,Matumizi ya Karafuu kwa kiwango kikubwa sana huweza kuleta athari kwenye Ini.

#Soma Zaidi Madhara ya Karafuu Mwilini,Hapa

4. Karafuu huweza kukulinda dhidi ya Saratani,

Baadhi ya Tafiti zinaonyesha Mafuta ya Karafuu husaidia ulinzi dhidi ya Saratani, Hasa hasa kwa Sababu ya antioxidants hii ya eugenol,

Tafiti zinaonyesha eugenol huzuia Saratani ya matiti kwa kuhamasisha Zaidi seli zenye Saratani kufa Zaidi na kuacha zile zenye afya.

5. Karafuu huweza kuua Viini vya magonjwa kama vile bacteria,

Karafuu zina tabia ambayo kitaalam tunasema antimicrobial properties, hii ina maana Karafuu huweza kuzuia ukuaji wa viini vya magonjwa kama vile bacteria.

Hivo basi,Kwa kujumuisha na njia nyingine za Usafi wa kinywa karafuu huweza kusaidia kwenye afya ya Kinywa na Meno, kama ukiitumia wakati wa kusafisha kinywa.

6. Karafuu huweza kusaidia kuweka Sawa kiwango cha Sukari kwenye damu,

Karafuu inaweza kusaidia kudhibiti kiwango cha sukari kwenye damu,
Misombo inayopatikana kwenye karafuu inaweza kusaidia kudhibiti sukari kwenye damu.

Kwa mfano, katika utafiti uliofanyika mwaka 2019 watu walio na prediabetes na wasio na ugonjwa wa kisukari ambao walitumia miligramu 250 (mg) ya karafuu kila siku kwa siku 30 walionyesha kiwango kidogo cha sukari kwenye damu baada ya kula.

Katika utafiti mwingine wa wanyama, nigricin, kiambato kinachopatikana kwenye karafuu, kiligundulika kuongeza uchukuaji wa sukari kutoka kwenye damu hadi kwenye seli, kuongeza utolewaji wa insulini, na kuboresha utendaji kazi wa seli zinazozalisha insulini kwenye panya.

7. Karafuu huboresha afya ya Mifupa,

Tatizo la Low bone mass ambalo hupelekea shida ya mifupa inayojulikana kama osteoporosis huwapata watu wengi, Mfano kwa nchi tu kama Marekani,inakadiriwa watu takribani Million 43 hupata shida hii kwa mujibu wa utafiti uliofanyika mnamo mwaka 2014.

Lakini, Tafiti zilizofanyika kwa wanyama,zilionyesha kwamba antioxidant ya eugenol kutoka kwenye Karafuu huweza kuboresha bone mass na kuzuia tatizo hili.

8. Karafuu huweza kusaidia kupunguza Vidonda vya Tumbo,

May reduce stomach ulcers
Tafiti nyingine za wanyama,zilionyesha Faida kubwa ya eugenol kutoka kwenye karafuu hata kwa kutibu Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo.

Hizo Ni baadhi ya FAIDA za KARAFUU tulizokuandalia kwa Siku ya Leo…!!!!

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass