Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
Magonjwa

JINSI YA KUSOMA KIPIMO CHA UKIMWI

JINSI YA KUSOMA KIPIMO CHA UKIMWI

Kama ilivyochangamoto kusoma kipimo cha Malaria au Mimba ndivo ilivyo changamoto katika kusoma kipimo cha ukimwi au kipimo cha HIV na kujua majibu sahihi kwa watu wengi.

Huku wengine wakizidi kuchanganyikiwa kuhusu Neno Positive na Negative. Wakishindwa kujua positive ni mtu ambaye ana ukimwi au hana, na Negative ni mtu ambaye ana ukimwi  au hana.

Wengine wakisoma majibu yao,wakikuta wataalam wa afya wametumia maneno mbali mbali kama Reactive na Non- reactive.

Katika Makala hii Utajifunza Jinsi ya Kusoma Kipimo cha Ukimwi au Kipimo cha HIV pamoja na baadhi ya maneno ambayo hutumika sana wakati wa Kutoa Majibu;

1. MANENO YANAYOTUMIKA NA MAANA ZAKE

✓ HIV POSITIVE- Hii ina maana kwamba aliyepima tayari ana maambukizi ya virusi vya Ukimwi

✓ HIV NEGATIVE- Hii ina maana kwamba aliyepima hana maambukizi yoyote ya virusi vya Ukimwi

✓ REACTIVE- Hii ina maana kwamba aliyepima tayari ana maambukizi ya virusi vya Ukimwi

✓ NON-REACTIVE- Hii ina maana kwamba aliyepima hana maambukizi yoyote ya virusi vya Ukimwi

2. JINSI YA KUSOMA KIPIMO CHA UKIMWI

– Baada ya kupima kipimo cha ukimwi au Kipimo cha HIV, majibu ya kipimo chetu hutegemea idadi ya mistari itakayojionyesha hapo kwenye Kipimo cha Ukimwi ambapo;

  • Kipimo cha Ukimwi au kipimo cha HIV kikionyesha Mstari Mmoja, ambapo tunasema mstari wa Control, Aliyepima hana maambukizi yoyote ya virusi vya ukimwi au ni NEGATIVE au NON-REACTIVE
  • Kipimo cha Ukimwi au kipimo cha HIV kikionyesha Mstari zaidi ya mmoja kama hapo kwenye picha yetu,Aliyepima tayari ana maambukizi ya virusi vya Ukimwi au ni POSITIVE au REACTIVE.
KUMBUKA: Lazima kipimo cha Ukimwi au Kipimo cha HIV kisome Mstari wa Control-C bila kujali ni Positive au Negative,

endapo umepima Kipimo cha Ukimwi au kipimo cha HIV na mstari wa C-control haujasoma, ujue kabsa umekosea kupima.

Hivo ndivyo tunavyosoma kipimo cha Ukimwi au kipimo cha HIV.

FAQs: Maswali yanayoulizwa mara kwa mara

Je, nini maana ya Positive na Negative kwenye kipimo cha Ukimwi au kipimo cha HIV?

✓ HIV POSITIVE- Hii ina maana kwamba aliyepima tayari ana maambukizi ya virusi vya Ukimwi

✓ HIV NEGATIVE- Hii ina maana kwamba aliyepima hana maambukizi yoyote ya virusi vya Ukimwi.

Je, ni lazima kipimo cha Ukimwi au kipimo cha Hiv kisome kwenye mstari wa C?

Ndyo,Lazima kipimo cha Ukimwi au Kipimo cha HIV kisome Mstari wa Control-C bila kujali ni Positive au Negative,

endapo umepima Kipimo cha Ukimwi au kipimo cha HIV na mstari wa C-control haujasoma, ujue kabsa umekosea kupima.

Hitimisho

Ni muhimu kufahamu hatua hizi za kupima Kipimo cha Ukimwi au kipimo cha HIV ili kupata Majibu sahihi na kuepuka kupata Majibu ya Uongo,

Lakini pia unahitaji kufahamu Zaidi kuhusu Ugonjwa wa Ukimwi,dalili zake,njia za maambukizi na Jinsi ya Kujikinga na Ugonjwa huu,

• Soma Zaidi hapa:Dalili za Ugonjwa wa UKIMWI

Wakati wa kufanya Kipimo cha Ukimwi au kipimo cha HIV,lazima ujue au Uzingatie mambo haya; kanuni sahihi za Upimaji,Muda wa kusoma majibu yako, expire date ya Kipimo, pamoja na muda wa kurudia vipimo baada ya vipimo vya Awali.

 

Dr.Ombeni Mkumbwa

Ushauri|Tiba|CheckIn ContactUs; +255758286584 or INBOX. For More Healthtips everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me Also Follow us on Instagram @afyaclass

3 Comments

  1. Hello habari ety Kama kipimo kikasoma c n huku kwengn kun mpauko w damu ina maana gani