Madhara na Tiba ya Maradhi ya Saratani
Saratani Ni Kikundi Cha Magonjwa Yanayojumuisha Ukuaji Wa Seli Usio Wa Kawaida Na Seli Hizo Hua Uwezo Wa Kuvamia Au Kuenea Kwa Sehemu Zingine Za Mwili. VIMBE ZA KAWAIDA AMBAZO HAZISAMBAI.
Saratani Inapoanza Mara Nyingi Haina Dalili Za Nje, Na Huchukua Muda Mtu Kugundua Endapo Ana Dalili Za Saratani Isipokua Tu Amefanya Vipimo.
Wengi Hugundua Saratani Baada Ya Kuwa Imeanza Kusambaa/Kuwa Sugu. Hii Hupelekea Matibabu Kuwa Magumu Na Kuchukua Muda Mrefu.
BAADHI YA AINA YA SARATANI
✓Saratani Ya Koo (Na kinywa)
✓Saratani Ya Mapafu,Figo,Ini
✓Saratani Ya Damu
✓Saratani Ya Ngozi
✓Saratani Ya Utumbo
✓Saratani Ya Matiti
✓Saratani Ya Shingo Ya Kizazi
✓Saratani Ya Tezi Dume
✓Saratani Ya Kibofu Cha Mkojo
Nk.
MADHARA YA SARATANI
Athari Za Mwili Na Akili:
✓Kushuka Kwa Kinga Za Mwili
✓Kupungukiwa Damu
✓Uchovu Sugu
✓Matatizo ya Uzazi
✓Shida Za Kiafya
✓Maumivu ya Mwili /Mifupa
✓Kudhoofu Kwa Mwili
✓Nywele Kunyonyoka
✓Kuharibika Ngozi
✓Kupoteza Uwezo Wa Kuona Vizuri Nk
Madhara Ya Muda Mrefu Huweza Kupelekea
✓Kupoteza Uwezo wa Kuzaa/Kuzalisha
✓Kuondolewa Kwa Baadhi Ya Organs Mwilini
MATIBABU YA MARADHI YA SARATANI
Upasuaji: Operesheni ambapo madaktari hukata tishu zilizo na seli za saratani.
Tiba ya kemikali: Dawa maalum zinazopunguza au kuua seli za saratani ambazo hatuwezi kuziona.
Tiba ya mionzi: Kutumia miale yenye nishati nyingi (sawa na X-ray) kuua seli za saratani.
Tiba ya homoni: Huzuia seli za saratani kupata homoni zinazohitaji kukua.
Immunotherapy: Tiba inayofanya kazi na mfumo wa kinga ya mwili wako ili kuusaidia kupambana na seli za saratani au kudhibiti athari zinazotokana na matibabu mengine ya saratani.