Asilimia 75 ya Vioo Kuuzwa nje ya Nchi
Rais Samia Suluhu Hassan ameweka jiwe la msingi la uzinduzi wa kiwanda cha kutengeneza vioo vya ujenzi cha Sapphire Float Glass kilichopo Mkuranga mkoani Pwani.
Rais Samia amesema kiwanda hicho kitazaa viwanda vingine hapo baadae na hata kufikia kutengeneza vioo vya magari.
Ameongeza kuwa asilimia 75 ya bidhaa za vioo zitakazotengenezwa kiwandani hapo zitauzwa nje ya nchi ili kuliingizia Taifa fedha za kigeni.
Kwa mujibu wa Rais Samia, kiwanda hicho kitaifanya Tanzania kuwa washiriki imara katika Soko Huru la Afrika kwa kupeleka bidhaa zake kwenye soko hilo.
Amewaagiza Viongozi wa mkoa wa Pwani kutumia fedha zitakazopatikana kutokana na uwekezaji huo katika kuboresha huduma kwa Wananchi na sio kuongeza viwango vya kulipana posho.