Hatari ya kupata Kisukari yaani Type 2 Diabetes
Hatari ya kupata Kisukari yaani Type 2 Diabetes
Vitu hivi huweza kuongeza hatari ya wewe kuwa na tatizo la kisukari hasa aina hii ya Type 2 Diabete,
1. UZITO MKUBWA- Tatizo la kuwa na Uzito Mkubwa yaani Overweight/Obesity
2. UMRI MKUBWA- Kuwa na Umri wa Kuanzia Miaka 45 na kuendelea
3. MLO/CHAKULA- je kila Siku unakula chakula cha aina gani?, je unakula vyakula vya sukari sana,mafuta sana n.k,
je unakula mlo kamili kila siku,au unakula mlo wenye virutubisho vya aina moja kama Vile Wanga kwa kiasi kikubwa n.k
4. MTINDO WA MAISHA-mbali na chakula unachokula kila siku, Je unakunywa Pombe au Kuvuta Sigara?
Je wewe ni Mtu wa kuzingatia ufanyaji wa MAZOEZI Kila siku,
Kutokufanya Mazoezi,kunywa Pombe au Kuvuta Sigara Vyote hivi huweza kuchangia tatizo hili kutokea
5. FAMILY HISTORY- Je tatizo hili lipo kwenye Ukoo wako au Familia yako? Kama watu wako wa karibu wana shida hii,basi hata wewe unaweza kuwa nalo.