Kwa Ushauri na Tiba Juu ya Tatizo lolote linalokusumbua TUWASILIANE HAPA.

Bofya hapa
News

Rais wa Zanzibar Amwakilisha Rais Samia Cuba

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameondoka Zanzibar kuelekea Havana, Cuba, kumwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la 77 na China (G77+ China) utakaofanyika kuanzia tarehe 15 hadi 16 Septemba 2023.

Mkutano huo unalenga kukutanisha Mataifa yanayoendelea (Developing Countries) ili kujadili changamoto zinazoikabili dunia, hususan baada ya kuathiriwa na janga la UVIKO-19 na migogoro inayoendelea duniani, pamoja na vikwazo mbalimbali vya kiuchumi.

Hivyo, mkutano huo utajikita zaidi katika kutafuta njia bora za kujenga ustahimilivu kupitia maendeleo ya sayansi, teknolojia, na ubunifu ili kundi la G77 na China liweze kufikia malengo yake kwa pamoja.

Mkutano huu utaongozwa na kaulimbiu isemayo “Current Development Challenges: The Role of Science, Technology and Innovation.”

Rais Dkt. Mwinyi anatarajiwa kutoa hotuba katika mkutano huo na kuelezea vipaumbele vya Tanzania, pamoja na hatua zilizochukuliwa kukuza utafiti na kuimarisha matumizi ya sayansi, teknolojia, na ubunifu (STI) katika kuleta mapinduzi ya kiuchumi.

DailyStories

Karibu DailyStories Kwa Taarifa Zote Muhimu ndani na Nje. More Updates everyday Link In http://cdp.pvh.mybluehost.me  Also Follow us on Instagram @afyaclass

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.