DALILI ZA OVARIAN CYSTS(VIUVIMBE KWENYE MIFUKO YA MAYAI)
OVARIAN CYSTS
• • • • • •
Dalili Za Ovarian Cysts
Ovarian cysts nyingi hazitambuliwi na hupotea zenyewe bila hata mwanamke mwenyewe kujua kuwa alikuwa nazo. Wakati cysts zinaonyesha dalili, maumivu maeneo ya tumbo au kwenye nyonga hujitokeza. Maumivu haya husababishwa na:
. kupasuka kwa cyst,
. ukuaji wa haraka na kunyumbuka,
. damu kutoka kwenye cyst,
. kujinyonga kwa cyst kwenye mishipa ya damu (torsion).
Kama cyst imekuwa kubwa, dalili nyingine huweza kujitokeza kutokana na msukumo au kujinyonga kwa viungo vingine vya mwili vilivyo karibu (torsion). Endapo ovari itajinyonga au kuhama kutoka sehemu yake ya awali, mtiririko wa damu kuelekea kwenye ovari hukatwa, na kama hakuna tiba itakayotolewa, tishu za ovari zinaweza kuharibika au kufa. Ovarian torsion inachangia asilimia 3 ya upasuaji wa dharura wa viungo vya uzazi vya akina mama. Katika mazingira hayo dalili hizi zinaweza kujitokeza:
. kujaa kwa tumbo, kutanuka tumbo,
. maumivu eneo la chini ya mgongo,
. chakula kutomeng’enywa tumboni,
. kusikia umeshiba baada ya kula chakula kidogo tu
. kusikia haja ndogo kwa ghafla
. kushindwa kumaliza kabisa haja ndogo
. Kujisikia haja kubwa kila wakati
. kupata haja kubwa kwa shida
. maumivu wakati wa tendo la ndoa